Arusha:Watuhumiwa wa Ugaidi wagoma kupandishwa kizimbani wakidai mpaka upelelezi utakapo kamilika
NA MICHAEL NANYARO
Mahakama kuu kanda ya Arusha imelazimika kuahirisha kesi ya ugaidi inayowakabili jumla ya watu 61 ambayo ilikuwa imepangwa kufanyika leo mahakamani hapo kufuatia watuhumiwa hao na kugoma kufika mahakamani,kwa madai kuwa wamechoka kupigwa tarehe na wanataka kesi yao ifanyiwe upelelezi pindi upelelezi huo utakapo kamilika nao wataweza kufika mahakamani.
Mahakama kuu kanda ya Arusha imelazimika kuahirisha kesi ya ugaidi inayowakabili jumla ya watu 61 ambayo ilikuwa imepangwa kufanyika leo mahakamani hapo kufuatia watuhumiwa hao na kugoma kufika mahakamani,kwa madai kuwa wamechoka kupigwa tarehe na wanataka kesi yao ifanyiwe upelelezi pindi upelelezi huo utakapo kamilika nao wataweza kufika mahakamani.
Katika kesi
hiyo ambayo inawakabili jumla ya watu 61 kwa tuhuma za ugaidi waliweza kufika
watuhumiwa tisa miongoni mwao mwanamke akiwa mmoja kati ya idadi ya watuhumiwa hao ambapo kwa
mujibu wa hakimu mkazi wa mahakama hiyo hakimu Gwantwa Mwankuga ameeleza
mahakamani hapo kuwa walipokea taarifa kutoka magereza kuu Kisongo kuwa baadhi
ya watuhumiwa waligoma kwenda mahakamani wakidai kuchoshwa na kupigwa tarehe za
shauri lao.
No comments